Michuano ya soka ya timu za mataifa ya Afrika Mashariki na kati kwa upande wa wanawake inatarajiwa kuanza leo mjini Kigali nchini Rwanda ambapo jumla ya timu tano zinatarajiwa kushiriki.
Timu zinazoshiriki ni wenyeji Rwanda, Uganda, Kenya, Ethiopia na Tanzania ambao ndiyo mabingwa wa mashindano kama haya yaliyofanyika mwaka 2016 nchini Kenya.
Katika siku ya kwanza leo, kufanyika mechi mbili za ufunguzi ambapo Rwanda itacheza dhidi ya Tanzania, mechi itakuwa kati ya Kenya na Uganda.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |