Maonesho ya filamu za China barani Afrika yaliyoandaliwa na Ofisi ya habari ya Baraza la serikali la China na Kituo kikuu cha Radio na Televisheni cha China, yamezinduliwa rasmi mjini Cape Town, Afrika kusini.
Akihutubia ufunguzi wa maonesho hayo, mwenyekiti wa zamu wa Kamati ya fedha za umma ya Jumuiya ya kiuchumi ya nchi za kusini mwa Afrika SADC Bw. Nthabiseng Khunou, amesema maonesho hayo yatawaburudisha watazamaji wa Afrika kwa filamu za China, na kuwafanya watu wa pande hizo mbili wawe karibu zaidi.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |