Rais wa Rwanda Paul Kagame na Xi Jingping walisaini makubaliano hayo mjini Kigali ikiwa ni pamoja na kwenye sekta za biashara, uchukuzi, miundo mbinu, uwekezaji, ngunvu kazi sayansi na teknolojia.
Aidha China itafadhili upanuzi wa hospitali ya wilaya ya Masaka ambayo ilijengwa kwa msaada wa China na pia kutoka mikopo ya ujenzi wa barabara ya kilomita 66 ya Huye-Kibeho-Munini pamoja na ile ya Bugesera inayoelekea uwanja wa ndege.
Rais Xi ameitaja Rwanda kama nchi imara na imepiga hatua kubwa kimaendeleo.
Sasa Rais Xi yuko nchini Afrika Kusini ambako anahudhuria mkutano wa 10 wa nchi za BRICS.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |