Shirikisho la soka duniani FIFA limemwacha nyota wa klabu ya PSG na timu ya taifa ya Brazil Neymar Jr kwenye orodha ya wachezaji 10 wanaowania tuzo ya mchezaji bora wa dunia kwa mwaka 2018.
Katika orodha ya majina 10 yaliyotajwa leo na FIFA nyota huyo hajajumuishwa, hali ambayo imezua mijadala mbalimbali kwa wadau wa soka wengine wakiunga mkono uamuzi wa FIFA na wengine wakipinga kuwa alistahili kuwepo kwenye orodha hiyo.
Orodha ya wanaume
Cristiano Ronaldo - Juventus na Ureno
Kevin De Bruyne - Manchester City na Ubelgiji
Antoine Griezmann - Atletico Madrid na Ufaransa
Eden Hazard - Chelsea na Ubelgiji
Harry Kane - Tottenham na England
Kylian Mbappe - Paris St-Germain na Ubelgiji
Lionel Messi - Barcelona na Argentina
Luka Modric - Real Madrid na Croatia
Mohamed Salah - Liverpool na Misri
Raphael Varane - Real Madrid na Ufaransa
Tuzo hiyo kwa msimu uliopita ilitwaliwa na Cristiano Ronaldo na kuwashinda mpinzani wake Lionel Messi aliyeshika nafasi ya pili na Neymar Jr aliyeshika nafasi ya pili. Kwa upande wa makocha wa kiume tuzo hiyo ilichukuliwa na Zinedine Zidane.
FIFA pia wametoa orodha ya majina ya wachezaji wanaowania tuzo hiyo kwa upande wa wanawake, na orodha ya makocha wanaowania tuzo ya ubora kwa mwaka 2018.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |