Rais Edgar Lungu wa Zambia anatarajiwa kuhudhuria mkutano wa kilele wa kundi la nchi za Brazil, Russia, India, China na Afrika Kusini (BRICS) unaofanyika nchini Afrika Kusini.
Waziri wa mambo ya nje wa Zambia Joseph Malanji amesema, akiwa nchini Afrika Kusini, rais Lungu anatarajiwa kufanya mazungumzo ya pande mbili na rais Vladmir Putin wa Russia na rais Recep Tayyip Erdogan wa Uturuki.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |