Ndege moja ya abiria ya shirika la ndege la Mexico iliyokuwa na abiria zaidi ya mia moja, imeanguka katika jimbo la Durango, kaskazini mwa Mexico. Wizara ya uchukuzi ya Mexico imesema ndege hiyo aina ya Embraer 190 iliyokuwa inaelekea Mexico City, ilianguka muda mfupi baada ya kuruka kutoka uwanja wa ndege wa kimataifa wa Durango, na kwamba hakuna vifo vilivyoripotiwa kwenye ajali hiyo.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |