Serikali ya Nigeria imekanusha uvumi kuwa operesheni ya idara ya huduma za nchi DSS imekamata fedha na silaha hatari kutoka nyumbani kwa mkurugenzi wa idara hiyo aliyefukuzwa kazi, na video inayoenea kuhusu suala hilo. Msemaji wa idara ya polisi wa siri Tony Opuiyo ametoa taarifa akisema, video hiyo ni ya feki.
Msemaji huyu amesema, hakuna operesheni kama hiyo iliyofanywa na polisi wa kupambana na ufisadi au idara nyingine ya usalama, katika ofisi ya DSS au nyumba ya mkurugenzi wa zamani wa idara hiyo.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |