• Idhaa ya Kiswahili
  • Uchumi
  • Michezo
  • Facebook
  • ChinaABC
  • Sayansi
  • Afya
  • Bei ya petrol yaongezeka wakati serikali ikijiandaa kuweka ushuru wa VAT kwa bidhaa hiyo kuanzia mwezi Septemba

    (GMT+08:00) 2018-08-15 19:54:12
    Wamiliki wa magari nchini Kenya kuanzia mwezi ujao watalazimika kutumia fedha nyingi zaidi baada ya Tume ya kudhibiti Nishati nchini humo (ERC) kuongeza bei ya rejareja ya petrol kwa Sh1.50.

    Ongezeko hili la bei linakuja kama kionjo tu kwa bidhaa zote za petroli kwani kuanzia mwezi ujao Hazina ya Taifa itaanza kutoza ushuru wa thamani kwa petrol,hivyo bei hiyo inatarajiwa kuongezeka zaidi.

    Kulingana na muongozo wa bei unaotolewa na ERC kila mwezi,uliotolewa tarehe 14 Agosti,petrol sasa itauzwa Sh113.73 jijini Nairobi,kutoka Sh112.2 mwezi uliopita.

    Watumizi wa mafuta ya dizeli watapata nafuu kiasi,huku lita moja ya bidhaa hiyo ikipungua kwa senti 51 hadi Sh102.74.

    Nyumba zinazotegemea mafuta ya taa pia zitapata afueni baada ya tume ya ERC kupunguza bei ya mafuta hayo kwa senti 78 hadi Sh84.95 kwa lita.

    Webradio
    Sauti
    6:00-7:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 1
    12:00-13:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 2
    20:00-22:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 3A
    • FM 3B
    Maoni yako