Mafunzo ya siku mbili ya mchezo wa mpira wa kikapu mpya unao julikana kwa jina ''Three on Three" yamekamilika huku vilabu mbali mbali vikishiriki kwenye mafunzo hayo yaliofanyika Viwanja vya Polisi Ziwani Mjini Unguja.
Akizugumza baada ya kukamilika mafunzo hayo ya siku mbili Mwenyekiti wa Chama cha mpira wa Kikapu Zanzibar (BAZA) Salmini Ramadhan Taso amesema lengo la mafunzo hayo ni kuwafundisha wachezaji hawa aina nyingine ya mpira wa kikapu.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |