Timu ya taifa ya soka ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, (The Leopards) ipo jijini Monrovia nchini Liberia, kwa maandalizi ya mchuano muhimu kufuzu kucheza fainali ya mataifa bingwa barani Afrika mwaka 2019 nchini Cameroon.
Kwa mara ya kwanza leo, kikosi hicho cha wachezaji 22 kimeanza kufanya mazoezi pamoja.
Kipa Ley Matampi Mvumi, hatakuwepo katika mchuano huo muhimu siku ya Jumapili kwa sababu klabu yake ya TP Mazembe haikumpa nafasi ya kuondoka kwa wakati na sasa nafasi yake imechukuliwa na Joel Kiassumbua.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |