Ubalozi wa China nchini Sweden leo umetoa taarifa ikieleza kushangaa na kukasirika na polisi wa nchi hiyo kutenda vibaya raia watatu wa China, na kulaani vikali kitendo hicho.
Habari zinasema wachina hao watatu ambao ni familia moja tarehe 2 alfajiri walifika nchini Sweden kufanya utalii, na walibishana na wafanyakazi wa hoteli yao baada ya kukataliwa kupewa vyumba. Polisi waliwashikilia kimabavu garini na kuwashusha kwenye makaburi yaliyoko mbali na mji.
Hadi sasa serikali ya Sweden bado inakaa kimya bila kutoa majibu yoyote.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |