Wizara ya mambo ya nje ya Syria na ya Iran zimetoa taarifa ya kuzipongeza Russia na Uturuki kwa kusaini makubaliano ya kuanzisha eneo lisilo na mapambano katika jimbo la Idlib, nchini Syria.
Wizara ya mambo ya nje ya Syria imesema, makubaliano hayo ni matokeo ya mazungumzo mengi na uratibu kati ya Syria na Russia.
Aidha, wizara ya mambo ya nje ya Iran imesema, kitendo hicho cha marais wa Russia na Uturuki ni hatua kubwa kwa kuondoa wapiganaji wa kigaidi jimboni humo.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |