Mkutano wa mwaka 2018 wa Baraza la haki za binadamu la Beijing uliofuatilia uondoaji wa umaskini ulifungwa jana Jumatano.
Mkutano huo wa siku mbili ulihudhuriwa na maofisa, wasomi na watu mashuhuri zaidi ya 200 kutoka nchi, sehemu na mashirika ya kimataifa 50, ambao walipeana maoni juu ya masuala ya kuondokana na umaskini na haki ya kuishi na kupata maendeleo, pamoja na uzoefu wa China katika kupunguza umaskini, ushirikiano wa kimataifa katika kupunguza umaskini, jitihada za kujenga jumuiya ya binadamu yenye hatma ya pamoja na umuhimu wake katika kulinda haki za binadamu.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |