Watu wapatao elfu 7 wamerudi nyumbani mkoani Idlib, kaskazini magharibi mwa Syria katika siku mbili zilizopita baada ya Russia na Uturuki kufikia makubaliano yanayolenga kuzuia makabiliano ya kijeshi mkoani humo. Umoja wa Mataifa umesema zaidi ya watu elfu 30 wamekimbia makazi yao kutokana na hofu na mashambulizi makali mkoani Idlib, ikiwa ni ngome ya mwisho ya waasi nchini Syria.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |