Timu za taifa za mpira wa kikapu za Nigeria na Tunisia zimefanikiwa kukata tiketi za kushiriki katika michuano ya dunia ya mpira wa kikapu itakayofanyika mwakani nchini China.
Timu hizo zimemaliza michezo yake katika makundi yake bila kupoteza mechi yoyote na kufanya timu hizo kuwa za kwanza kukata tiketi hizo za kuwakilisha bara la Afrika katika michuano hiyo. Zinabaki nafasi 3 tu za Bara la Afrika.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |