Katika mbio za marathon za Cape Town zilizofanyika jana nchini Afrika Kusini, wanariadha kutoka Afrika Mashariki wamefanikiwa kushinda nafasi ya pili, ambapo kwa upande wa wanawake, Failuna Matanga kutoka Tanzania alishinda nafasi ya pili kwa kutumia saa 2 na dakika 30 na nafasi ya kwanza ikichukuliwa na Helalia Johannes kutoka Namibia aliyetumia saa 2 na dakika 28.
Kwa upande wa wanaume Albert Korir kutoka Kenya alishika nafasi ya pili kwa kutumia saa 2, dakika 9 na sekunde 2 nyuma ya Stephen Mokoka wa Afrika Kusini aliyeshinda nafasi ya kwanza kwa kutumia saa 2 dakika 8 na sekunde 31.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |