Michuano ya ligi kuu Zanzibar ya mpira wa mikono inatarajia kutimua vumbi kuanzia Oktoba mosi katika viwanja vya jeshi nyuki visiwani Zanzibar.
Kwa mujibu wa taarifa ndani ya chama cha mpira wa mikono Zanzibar (ZAHA) kupitia msemaji wake Ameri Khalid amesema ligi itahusisha madaraja ya vijana wakubwa, wanaume na wanawake kutoka Unguja na Pemba.
Kwa upande mwengine amesema Timu hizo za Zanzibar zitatumia mashindano hayo kujindaa na mashindano ya Afrika Mashariki na kati yatakayofanyika ndani ya visiwa vya Zanzibar kwa mara ya kwanza mwezi wa Disemba.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |