Katika mechi inayofahamika kutokana na mkubwa nchini Tanzania, kati ya watani wa kihistoria Simba na Yanga, jana imeisha kwa matokeo ya bila kufungana licha ya jitihada zilizofanywa na kila upande.
Simba ambao walipewa nafasi kubwa ya kushinda mechi hiyo msimu huu, kitakwimu walifanikiwa kulisakama lango la wapinzani wao, na sifa anuai zikimwendea mlinda mlango wa Yanga Beno Kakolanya ambaye alimudu jukumu lake dhidi ya mashambulizi.
Katika ligi kuu msimu huu, hii ni sare ya pili kwa Simba na ikiwa ni sare ya kwanza kwa Yanga katika mechi tano ilizocheza.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |