Mwanadiplomasia wa China nchini Kenya Bw. Li Xuhang amewapongeza wafanyakazi wanaojenga reli ya SGR kutokana na juhudi zao bila ya kusita hata wakati wa siku ya taifa ya China, ili kuhakikisha reli hiyo inafanya kazi kwa utaratibu.
Bw. Li amesema tarehe 1 Oktoba ambayo ni siku ya taifa ya China ni moja kati ya siku muhimu za mapumziko nchini China, na kwamba kazi ya kujitolea ya wafanyakazi wa reli ya SGR itasaidia kuimarisha ushirikiano kati ya China na Kenya, na maendeleo ya kijamii na kiuchumi nchini Kenya.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |