Baraza la usalama la Umoja wa mataifa limeamua kuongezea muda hatua za kukagua meli kwenye pwani ya Libya kwa miezi 12 zaidi, ili kupambana na magendo ya wahamiaji.
Kwa mujibu wa azimio Namba 2437 la baraza hilo, nchi wanachama wa Umoja wa mataifa wanaruhusiwa kukagua meli zinazoshukiwa kutumiwa kusafirisha kiharamu wahamiaji kutoka Libya, na kuzikamata meli zilizothibitishwa kuhusika na shughuli hizo.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |