Ligi ya mabingwa barani ulaya imeendelea usiku wa kuamkia leo, kwa timu za makundi kadhaa kukutana, kundi A, Atletico Madrid imeibuka na ushindi wa magoli 3-1 dhidi ya Club Brugge, na Borussia Dotmund wameifunga Monaco goli 3-0.
Kundi B, PSV Eindhoven imekubali kichapo cha 2-1 toka kwa Inter Milan, huku Barcelona ikiifunga Tottenham Hotspurs 4-2.
Kundi C, PSG imeichakaza FK Creva Zvezda kwa goli 6-1, Neymar akipiga hat trick. Nayo Napoli imeilaza Liverpool kwa goli 1-0.
Kundi D, Schalke 04 imeipiga Lokomotiv Moscow bao 1-0 na Porto kuibuka kidedea kwa goli 1-0 dhidi ya Galatasaray.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |