Jumla ya magari 23 yanatarajiwa kushiriki mbio za magari zilizo kwenye ratiba ya shirikisho la mbio za magari barani Afrika. Mbio hizo zinafahamika kwa jina la "Rwanda Mountain Gorilla Rally 2018". Mbio za mwaka huu zitatimua vumbi kwa siku mbili kuanzia Oktoba 5 na kumalizika Oktoba 6 nchini Rwanda.
Shirikisho la mchezo huo nchini Rwanda (RAC) kupitia katibu wake mkuu bwana Ange Cyatangabo amethibitisha mbio za mwaka huu zitakuwa za kipekee na hadi sasa madereva waliosajiliwa nu kutoka Rwanda, Uganda na Burundi. Ujio mpya wa Giancarlo Davite ambaye ni mpinzani mkubwa wa Ruddy Canthanede ni kitu ambacho mashabiki wanakitegemea sana.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |