• Idhaa ya Kiswahili
  • Uchumi
  • Michezo
  • Facebook
  • ChinaABC
  • Sayansi
  • Afya
  • Mpango wa kuondoa dola za kimarekani katika uchumi wawasilishwa kwa serikali ya Russia

    (GMT+08:00) 2018-10-05 09:39:32

    Waziri wa fedha wa Russia Bw. Anton Siluanov amesema mpango wa kuondoa dola za kimarekani kwenye uchumi wa Russia umeandaliwa na kuwasilishwa kwa serikali.

    Bw. Siluanov amesema mpango huo unawataka wauzaji nje kutumia ruble ya Russia badala ya dola ya kimarekani kwenye miamala ifikapo mwaka 2024.

    Msemaji wa Ikulu ya Russia Bw. Dmitry Peskov amesema mchakato wa kuondoa dola za kimarekani kwenye uchumi wa Russia ni mgumu na utachukua muda mrefu, na hakuna mipango ya kuacha kabisa matumizi ya dola za kimarekani kwenye miamala.

    Webradio
    Sauti
    6:00-7:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 1
    12:00-13:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 2
    20:00-22:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 3A
    • FM 3B
    Maoni yako