Serikali ya Tanzania imeiagiza bodi ya utalii ya Tanzania TTB ifanye juhudi zaidi kutangaza vivutio vya utalii.
Naibu waziri wa rasilimali na utalii wa Tanzania Bw. Japhet Hasunga, amesema bodi ya utalii ya Tanzania TTB inapaswa kufanya uvumbuzi zaidi katika kuendeleza utalii nchini humo badala ya kulalamika ukosefu wa fedha. Amesema, ni bora wajaribu kutumia teknolojia mpya kama vile mitandao ya kijamii, katika kuhimiza watu wote wa Tanzania kushiriki kwenye maendeleo ya utalii ya nchi hiyo.
Pia Bw. Hasunga amesema, fedha za kazi hiyo zinapaswa kutumia kama ilivyopangwa, na kuonya kuhusu matumizi mabaya ya fedha na raslimali.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |