Kampuni ya magari Isuzu East Africa imeanzisha kituo kipya cha kurekebisha magari mjini Nairobi.
Kituo hicho kilichojengwa kwa gharama ya dola milioni 1 kitawezesha wateja kupata huduma na vipuli kwa bei nafuu.
Mkurungezi wa Isuzu East Africa Rita Kavashe amesema kapuni hiyo iko tayari kuendelea kutoa huduma za kiwango cha kimataifa kwa wateja wake kwa bei nafuu.
Isuzu pia imesema inatarajia kufungua vituo vingine viwilli kwenye ushoroba wa uchukuzi wa Mombasa-Malaba kati ya sasa na mwaka 2020.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |