Benki ya Dunia imesema inapanga kutenga Shilingi ya Tanzania trilioni 1.357, sawa na dola za kimarekani milioni 59.4 kuunga mkono sekta ya elimu nchini Tanzania. Mkurugenzi wa Benki ya Dunia nchini Tanzania, Malawi na Somalia Bibi Bella Bird ametoa ahadi hiyo baada ya kukutana na rais John Magufuli katika ikulu mjini Dar es Salaam. Kwa mujibu wa taarifa ya Kurugenzi ya Mawasiliano ya Rais, Bibi Bird na rais Magufuli walipitia maendeleo katika miradi inayofadhiliwa na Benki ya Dunia kwa nchi hiyo, na utekelezaji wa miradi mingi unaendelea vizuri.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |