Rais Donald Trump wa Marekani amesema atamteua balozi mpya wa nchi hiyo kwenye Umoja wa Mataifa katika wiki mbili au tatu zijazo, ili kuchukua nafasi ya Bibi Nikki Haley aliyejiuzulu. Bibi Haley ataendelea na wadhifa huo hadi mwishoni mwa mwaka huu, ambapo atamaliza muda wake wa kuhudumia kwa miaka miwili. Rais Trump alisema Haley alimwambia kuhusu kujiuzulu kwake miezi sita iliyopita.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |