Mahakama ya Katiba nchini Cameroon imepokea madai kutoka kwa wagombea watatu wa upinzani wakitaka uchaguzi wa rais uliofanyika Oktoba 7 ufutwe.
Tume ya Uchaguzi nchini humo imesema, jumla ya malalamiko 25 yamewasilishwa na wapiga kura na wagombea, wakitaka aidha sehemu au uchaguzi wote kufutwa.
Hata hivyo, chama tawala nchini Cameroon (CPDM) kimetoa wito wa utulivu wakati nchi ikisubiri kutangazwa kwa matokeo rasmi ya uchaguzi wa rais.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |