Waziri mkuu wa Israel Bw. Benjamin Netanuahu amelionya kundi la Hamas akisema litapata hasara kubwa kama litaendelea na mashambulizi ya kimabavu dhidi ya Israel katika uzio wa mpaka wa usalama katika Ukanda wa Gaza. Ijumaa iliyopita, waandamanaji elfu 15 walichoma matairi na kurusha mawe, vifaa vya milipuko na makombora dhidi ya askari wa Israel, na kwa mujibu wa ripoti za Palestina, waandamanaji watano waliuawa wakiwemo watatu waliojaribu kuvuka uzio na kufika kwenye kituo cha jeshi la Israel.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |