Baraza la mawaziri la Israel limeidhinisha kutenga dola za kimarekani milioni 6.1 kwa ajili ya ujenzi wa makazi mapya ya wayahudi huko Hebron, mji wa magharibi mwa Mto Jordan.
Vyombo vya habari nchini humo vimesema, hii ni mara ya kwanza katika miaka 16 iliyopita kwa Israel kujenga makazi ya wayahudi huko Hebron. Makazi hayo yatajengwa kwenye kituo cha zamani cha kijeshi cha Israel ambacho kiko karibu na barabara kuu ya Hebron. Makazi hayo yatakuwa na majengo 31 pamoja na shule ya chekechea
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |