• Idhaa ya Kiswahili
  • Uchumi
  • Michezo
  • Facebook
  • ChinaABC
  • Sayansi
  • Afya
  • Kenya: Wadau wataka kuimarishwa sekta ya ngozi

    (GMT+08:00) 2018-10-16 19:29:15
    Wadau kwenye sekta ya ngozi nchini Kenya wanaiomba serikali kuanzisha taasisi ya kutoa mafunzo kwa vijana kwenye sekta hiyo ili kuwasaidia kuongeza ujuzoi.

    Wamesema mafunzo hayo pia yatawasaidia kuanza kuzalisha bidhaa za ngozi za kiwango cha kimataifa.

    Wadau kwenye sekta hiyo wamekuwa wakilalamika kuwa ujuzi walio nao ni wa kimsingi tu na hivyo hawawezi kuiendeleza sekta yenyewe.

    Mapema mwaka huu baraza la maendeleo ya ngozi lilitaja usimamizi mbaya wa vichinjio kuwa sababu moja ya viwango vya chini vya ngozi.

    Licha ya kuwa Kenya ina ngozi ya kutosha lakini makampuni mengi yanaagizia kutoka nje ya nchi kwani kiwango cha nyumbani ni duni.

    Webradio
    Sauti
    6:00-7:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 1
    12:00-13:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 2
    20:00-22:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 3A
    • FM 3B
    Maoni yako