Kampuni ya mafuta ya Simba Essel Energy inasubiri idhini husika za serikali nchini Kenya ili kuanza utafutaji wa mafuta kaunti ya Wajir kaskazini mwa nchi hiyo.
Tathmini ya mwaka jana ilionyesha kuwa eneo hilo linaweza kuwa na hadi mapipa milioni 400 .
Wataalam wa kampuni hiyo watawasilisha maombi kwa wizara kawi na kusubiri idhini kabla ya kusaini makubaliano .
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |