Al Ahly ya Misri, itacheza na Esperance de Tunis, ya Tunisia, katika fainali ya kuwania taji la klabu bingwa barani Afrika, itakayofanyika mwezi Novemba.
Licha ya kufungwa mabao 2-1 na Entente Setif ya Algeria siku ya Jumanne usiku, ilifuzu kwa jumla ya mabao 3-2 kwa sababu ya ushindi wa nyumbani wa mabao 2-0 zaidi ya wiki tatu zilizopita.
Mabingwa hao mara nane wa taji hili, wataanza kuwa wenyeji wa mchuano wa fainali Novemba 2 jijini Cairo, kabla ya mechi ya mwisho kuchezwa mjini Rades, Novemba 9.
Esperance de Tunis, nayo ilifuzu baada ya kupata ushindi wa mbao 3-4. Licha ya kufungwa ngenini na Primero de Agostio bao 1-0, ikicheza nyumbani ilifanikiwa kupata ushindi wa manao 4-2.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |