• Idhaa ya Kiswahili
  • Uchumi
  • Michezo
  • Facebook
  • ChinaABC
  • Sayansi
  • Afya
  • Tanzania: Kampuni zafunzwa jinsi ya kusindika

    (GMT+08:00) 2018-11-01 19:01:59
    Shirika la Umoja wa mataifa la Maendeleo ya Viwanda (Unido), limeibua mradi kuwezesha kampuni za wazawa, kusindika mazao kwa kiwango cha ubora wa kimataifa ili kufikia soko la utalii.

    Kupitia mwakilishi wake nchini Tanzania Stephen Kargbo, unido imesema kuwa mradi huo utawawezesha wazalishaji kuja na bidhaa za ubora wa juu na unaostahili kwenye masoko ya utalii. Mradi huu utakaofadhiliwa na serikali ya Uswisi, unalenga kuzisaidia kampuni za wazawa kufikia kiwango cha ubora wa bidhaa cha kimataifa kinachostahili, ambacho ni ISO 22000.

    Naye mshauri wa kitaifa wa mradi huo kutoka Unido Vedastus Timothy, alisema watalii wanataka kutumia bidhaa zilizozalishwa na kusindikwa nichi Tanzania, bora tu ziwe salama na zenye ubora wa kimataifa. Wasindikaji waliopewa mafunzo wameombwa kuwafunza wenzao ili kusindika bidhaa kwa viwango vya ubora wa kikanda, kitaifa na kimataifa.

    Webradio
    Sauti
    6:00-7:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 1
    12:00-13:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 2
    20:00-22:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 3A
    • FM 3B
    Maoni yako