Baada ya matokeo ya kundi A hadi D mechi zilizochezwa juzi, jana mechi za makundi mengine ziliendelea, ambapo
kundi E: FB Bayern Munchen imetoka na ushindi wa 2-0 dhidi ya AEK Athens, Benfica wao wametoka sare ya 1-1 na Ajax.
Nayo Lyon imemaliza kwa sare ya 2-2 na Hoffenheim, huku Manchester city imefanya mauaji kwa kuichapa Shakhtar Donetsk 6-0 katika kundi F.
kundi G: CSKA Moscow imekubali kipigo cha 2-1 toka kwa Roma, nayo Real Madrid imetoa kipigo cha mbwa mwizi cha 5-0 kwa Victoria Plzen, na michezo ya kundi H, Valencia imeifunga Young Boys 3-1 huku Manchester United ikiibuka na ushindi wa 2-1 dhidi ya Juventus.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |