• Idhaa ya Kiswahili
  • Uchumi
  • Michezo
  • Facebook
  • ChinaABC
  • Sayansi
  • Afya
  • AFCON2019: CAF yafyekelea mbali mechi ya Harambee Stars na Sierra Leone

    (GMT+08:00) 2018-11-13 09:14:23

    Shirikisho la soka barani Afrika (CAF), imefutilia mbali mechi ya kundi F ya kusaka tiketi ya kufuzu kwa kombe la mataifa ya Afrika (FACON2019) kati ya Kenya na Sierra Leone iliyopangwa kufanyika Novemba 18 uwanja wa Kasarani jijini Nairobi.

    Uamuzi wa CAF umetolewa siku 6 kabla ya mtanange huo, unatokana na wapinzani wa Kenya, Sierra Leone kukosa sifa ya kucheza mchezo huo kwasababu bado wanatumikia kifungo cha shirikisho la soka duniani (FIFA) na shirikisho la soka Afrika (CAF), uamuzi wa mwisho kuhusu mustakabali wa kundi F utatolewa hivi karibuni.

    Kenya inaongoza kundi hilo kwa kuwa na pointi 7, pointi 4 mbele ya Ghana ainyoshika nafasi ya pili, na Ethiopia inayoshika nafasi ya tatu.

    Webradio
    Sauti
    6:00-7:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 1
    12:00-13:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 2
    20:00-22:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 3A
    • FM 3B
    Maoni yako