Kwa upande wa wanawake mshindi wa mbio hizo ni Medine Armino wa Ethiopia aliyetumia saa 2:29.30 akifuatiwa na Nazret Gebrehiwet wa Eritrea 2:29.30 huku nafasi ya tatu ikienda kwa Muethiopia mwingine Selamawit Tsegaw aliyemaliza kwa saa 2:31.40.
Kwa upande wa wanaume mshindi aliibuka Mohamed El Aaraby kutoka Marta aliyetumia saa 2:10.41 akifuatiwa na Mganda Felix Chemonges 2:11.54 huku nafasi ya tatu ikienda kwa Deresa Ulfata wa Ethiopia aliyetumia saa 2:12.31.
Washindi wa mbio hizo wataingia katika shindano la kufuzu kwa mashindano ya dunia yatakayofanyika Doha Qatar mwakani.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |