Katibu mkuu wa kamati ya utendaji ya Chama cha Ukombozi cha Wapalestina PLO Bw. Saeb Erekat amesema mswada wa azimio wa Marekani unaolikosoa kundi la Hamas kuchochea mabavu na kurusha roketi dhidi ya Israel uliowasilishwa kwenye Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa unakwenda kinyume na ukweli. Ametoa wito kwa jumuiya ya kimataifa kukabiliana na "hatua za utawala wa rais Donald Trump wa Marekani."
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |