Rais Emmanuel Macron wa Ufaransa aliye ziarani nchini Ujerumani ametoa wito wa kuijenga Ulaya iwe na umoja, nguvu zaidi na uhuru. Akiwahutubia wabunge wa Ujerumani katika hafla ya kuadhimisha Siku ya Ujerumani ya Kuomboleza wahanga wa vita na mgogoro, rais Macron amesema Ulaya inakabiliwa na changamoto mbalimbali kama vile mabadiliko ya hali ya hewa, migogoro ya kibiashara na uhamiaji, Ufaransa na Ujerumani zina wajibu wa kuzuia dunia isiingie kwenye ghasia.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |