Rais Emmanuel Macron wa Ufaransa amefafanua tena wazo la kujenga ulinzi wa Ulaya, na kusema utakuwa wa kujitegemea, wenye nguvu, na umoja zaidi.
Rais Macron amesema hayo wakati wa ziara yake nchini Ubelgiji, ambapo amefanya mazungumzo na waziri mkuu wa Ubelgiji Bw. Charles Michel katika Chuo Kikuu cha Catholique de Louvain. Pia amejadiliana na wanafunzi wa chuo kikuu cha Ubelgiji kuhusu ulinzi wa Ulaya, sera ya kubana matumizi, mgogoro wa uhamiaji na masuala mengine ya Umoja wa Ulaya na kimataifa.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |