Umoja wa Mataifa umetoa wito kuongeza ushirikiano wa kimataifa kupambana na uhalifu dhidi ya wanyamapori na wa kimataifa.
Mkurugenzi wa idara ya kupambana na dawa za kulevya na uhalifu ya Umoja wa Mataifa UNODC Bw. Miwa Kato amesema, uhalifu dhidi ya wanyamapori unaoathiri uanuwai wa viumbe na maendeleo, ni uhalifu wa kimataifa wenye hatari ya chini na faida kubwa. Hakuna nchi moja peke yake inayoweza kuzuia uhalifu huo.
Katibu wa kwanza wa wizara ya utalii na wanyamapori ya Kenya Bibi Margaret Mwakima pia ametoa wito wa ushirikiano wa kimataifa katika kulinda wanyama na mimea inayoharibiwa kutokana na tamaa, ubinafsi, ufuatiliaji wa mali na kupuuza sheria.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |