Kampuni ya mawasiliano nchini Kenya Safaricom imetangaza zawadi ya data kwa wateja wake kwa jina "Asante Data Sunday".
Chini ya mpango huo wateja watarejeshewa data yote waliotumia 23 na 24 Novemba siku ya Jumapili.
Mkurungezi wa kitengo cha wateja kwenye kampuni hiyo Charles Kare amesema zawadi hiyo itakuwa ni sehemu ya kusherehekea miaka 18 ya kampuni hiyo
Amesema imani ya zaidi ya wateja milioni 17 wa kampuni hiyo ndio imeiwezesha kufikia kiwango cha kimataifa na hivyo haina budi kuwatambua kila mara.
Ili kupokea data wateja watabonyeza *444*20#.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |