Zimbabwe imeshusha makadirio ya ukuaji wa uchumi wake hadi kufikia asilimia 4 kwa mwaka 2018 kutoka asilimia 6.3 iliyokadiriwa awali kutokana na changamoto za kiuchumi katika robo ya pili ya mwaka huu.
Waziri wa uchumi wa Zimbabwe Bw. Mthuli Ncube alipowasilisha bajeti ya serikali ya mwaka 2019 kwenye bunge la Zimbabwe, amesema uchumi utaongezeka kwa asilimia 3.1 katika mwaka 2019, ikilinganishwa na asilimia 9 iliyokadiriwa awali kutokana na udhaifu wa kifedha na ukame unaokadiriwa kutokea katika msimu wa kilimo wa mwaka 2018/19.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |