Awali katika hatua ya mzunguko, Tanzania ilimaliza ikiwa kinara baada ya kushinda mechi zake zote tatu ikafuatiwa na Uganda waliomaliza wakiwa nafasi ya pili na pointi 6 na hivyo timu hizo kukutana katika fainali.
Kabla ya mchezo wa fainali, kulipigwa mchezo wa kusaka mshindi wa tatu kati ya Malawi iliyomaliza hatua ya mzunguko ikiwa nafasi ya tatu na Shelisheli iliyokuwa ikishika mkia.
Katika mashindano hayo mchezaji bora amekuwa Yahya Tumbo kutoka Tanzania, kipa bora ni Ibrahim Abdallah kutoka Tanzania, tuzo ya mfungaji bora imeenda kwa James Chikoka kutoka Malawi aliyemaliza na mabao 10 na kocha bora ni Boniface Pawasa kutoka Tanzania.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |