Rais Emmerson Mnangagwa wa Zimbabwe atafungua rasmi mkutano wa Teknolojia ya Mawasiliano (ICT) unaotarajiwa kuanza kesho mjini Harare, ambao utawakutanisha zaidi ya washiriki 500 kutoka nchi kadhaa za Afrika na wataalam wa TEKNOHAMA duniani.
Waziri wa elimu ya Msingi na Sekondari nchini Zimbabwe Bw. Paul Mavima amesema, mawaziri kutoka nchi 17 za Afrika na mashirika 45 ya kimataifa kama Microsoft na Intel wamethibitisha kushiriki.
Amesema mkutano huo unafanyika wakati serikali ya Zimbabwe inajitahidi kuifanya sekta ya elimu kuendana na mahitaji ya karne ya 21.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |