Wizara ya Mambo ya Nje ya Ukraine imeitaka Russia iwaachie huru wanamaji wa Ukraine wanaoshikiliwa kufuatia mivutano katika Bahari ya Azov, na kuhakikisha wanarudi nyumbani salama. Jumapili jeshi la Russia lilifyatua risasi na kukamata meli tatu za Ukraine karibu na Mlango Bahari wa Kerch unaotenganisha Bahari Nyeusi na Bahari ya Azov. Wakati huohuo, bunge la Ukraine limesema uchaguzi mkuu ujao wa Ukraine utafanyika tarehe 31, Machi mwakani kama ilivyopangwa.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |