• Idhaa ya Kiswahili
  • Uchumi
  • Michezo
  • Facebook
  • ChinaABC
  • Sayansi
  • Afya
  • Tanzania: Benki Kuu ya Tanzania yafungua benki tano kubadilisha fedha za kigeni

    (GMT+08:00) 2018-11-29 19:32:11
    Benki Kuu ya Tanzania (BoT) imezifungia kwa mwezi mmoja benki za kibiashara tano kutojihusisha na ubadilishaji wa fedha za kigeni kutokana na sababu ambazo bado hazijawekwa wazi.

    Hatua hiyo ya BoT inatazamwa kama mwendelezo wa chombo hicho kikuu cha usimamizi wa fedha kudhibiti biashara ya utakatishaji na ubadilishaji wa fedha kiholela.

    Takriban wiki mbili zilizopita BoT iliyafungia maduka kadhaa jijini Arusha kwa madai kuwa yanaendesha shughuli zake kinyume na sheria zinazosimamia biashara hiyo, baada ya hapo ilitangaza kuwa huduma za ubadilishaji fedha zitapatikana katika hoteli za kitalii, benki na ofisi zao.

    Webradio
    Sauti
    6:00-7:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 1
    12:00-13:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 2
    20:00-22:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 3A
    • FM 3B
    Maoni yako