• Idhaa ya Kiswahili
  • Uchumi
  • Michezo
  • Facebook
  • ChinaABC
  • Sayansi
  • Afya
  • Sudan Kusini yatangaza mlipuko wa homa ya manjano karibu na mpaka wa DRC

    (GMT+08:00) 2018-11-30 09:35:47

    Naibu waziri wa afya wa Sudan Kusini Bw. Makur Matur Koriom ametangaza kutokea kwa mlipuko wa homa ya manjano kusini magharibi mwa nchi hiyo karibu na mpaka wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo DRC.

    Bw. Koriom amesema, mgonjwa aliyeshukiwa kuambukizwa virusi vya Ebola kwenye kijiji cha Supiri, jimbo la Gbudue karibu na mpaka na DRC amethibitishwa kuambukizwa virusi vya homa ya manjano.

    Bw. Koriom amewashauri wakazi wa huko kukaa kwenye kijiji cha Supiri hadi matokeo ya upimaji yakatapotangazwa. Vilevile amewataka wasiende DRC isipokuwa kuna jambo la dharura.

    Webradio
    Sauti
    6:00-7:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 1
    12:00-13:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 2
    20:00-22:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 3A
    • FM 3B
    Maoni yako