Wiki ijayo Kenya itafanya kikao cha uchumi wa bara, kikao cha Afrika cha Utafiti wa Uchumi (AERC) kujadili mgogoro wa madeni unaokuja katika eneo hilo.
Kikao ambacho kinaanza Desemba 2 hadi 6 inatarajiwa kuleta pamoja zaidi ya watafiti 200, wasomi, watunga sera na wataalam wa masuala ya Kiuchumi ili kujadili masuala yanayohusiana na maendeleo ya kiuchumi ya Afrika.
Mkutano unakuja wakati ambapo nchi nyingi katika kanda ikiwa ni pamoja na Kenya iko na shinikizo kubwa la kupunguza kukopa.
Takwimu kutoka Benki ya Dunia inaonyesha kwamba nchi 18 za Afrika ziko na hatari kubwa ya dhiki ya madeni ikilinganishwa na nchi nane tu miaka mitano iliyopita.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |