Vitendo vya mabavu kote nchini Iraq vilisababisha vifo vya jumla ya raia 41 mwezi Novemba, idadi ambayo ni ndogo kushuhudiwa tangu Tume ya Msaada ya Umoja wa Mataifa nchini Iraq ianze kuchapisha takwimu za vifo kwa mwezi miaka sita iliyopita. Taarifa iliyotolewa na Tume hiyo imesema raia 73 walijeruhiwa katika mashambulizi ya kigaidi na migogoro nchini humo mwezi uliopita. Mji mkuu Baghdad uliathiriwa vibaya kwa kuwa na vifo vya watu 23 na wengine 32 kujeruhiwa.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |